MKASA WA KWELI NDANI YA NDOA 2
Baada ya dakika 45 PETER aliingia akiwa anahema kwa wasiwasi uliompata kutokana na yale ambayo niliyomueleza kuwa yametokea nyumbani kwake.Alimpita house girl ambaye alikuwa akiendelea kumbembeleza mtoto barazani na kuja moja kwa moja mpaka sitting room na kukaa karibu na mkewe huku akimuinua kichwa.JESCA ambaye baada ya kumuona mumewe ameingia na kumuinua kichwa huku akimuuliza kulikoni, alimsukuma mumewe na kutoa sauti kali iliambatana na maneno ambayo yalizidi kumchanganya PETER. "Niacheeee!unaniinua kichwa ili nikuambie nini!hivi makenika anaweza kuijua gari kuliko alieitengeneza kiwandani?Hivi mimi nitakuwa na la kuambia kuliko wewe ulietenda!unataka kusema hauzijuhi!au haukuziweka wewe!Umesahau kuwa umenioa nikiwa na degree yangu!unalipi la kuniambia!nini bahati mbaya!au ndio uovu wako unataka kumsingizia shetani!haya niambie kuwa shetani alikupitia!ili nikuulize kilichopelekea upange ahadi ya kukutana mpaka amekupitia!". JESCA alitokwa na maneno mfululizo bila hata y