MKASA WA KWELI NDANI YA NDOA 1
Ufuatao ni mkasa ambao umemtokea Jesca.Jesca ni binti wa
miaka 24 ambae ameolewa na Peter.Ni Miaka miwili sasa toka walipofunga
ndoa,katika muda wote wa maisha yao ya uchumba mpaka walipofunga ndoa waliishi
kwa upendo,Amani,mafanikio na Amani kubwa sana katika maisha yao.
Tabia zao ambazo walikuwa nazo kabla ya uchumba na hata
baada ya uchumba ziliwafanya wao,wazazi wao na hata wanafunzi wenzao katika
chuo walichokuwa wanasoma kuamini na kuwatabiria kuwa kila mmoja kati yao
amepata mtu sahihi.Mahusiano hayo yaliwapeleka katika uchumba ambao uliwafanya
situ mke na mume lakini pia uliwapa zawadi ya furaha kwao nayo ni motto pekee
wa kiume Herman,
Kutokana na mtoto huyo maisha yao yaliendelea kunawari kwa
maelewano na uaminifu mkubwa na hapakuwa na mabadiliko yoyote ambayo labda
yangeleta dosari au msukosuko katika ndoa yao yenye muda wa miaka miwili na
motto mmoja.
Hivi ni nani ambae asingependa maisha ambayo Jesca na Peter
waliishi? Maisha ya ndoa yanamisukosuko mingi lakini kubwa ambalo hufanya ndoa
nyingi zivunjike na ukosefu wa uaminifu na tamaa.Hili kwa kina JESCA na PETER
halikuwepo hata kidogo.Simu zao hazikuwa na password na wala haijawhi kutikea
mmoja wao kumkataza mwenzie kushika au kupokea simu ya mwenzake,lakini pia
haikuwahi kutokea mmoja wao kupigiwa simu na asipokee mbele ya mwanzake,maisha
yao yalijaa uaminifu wa hali ya juu na upendo usionakifani.
Maisha yao yaliwavutia wengi na hasa wale ambao waliokuwa na
migogoro katika ndoa zao,walishindwa kujua siri ya mafanikio ya wanandoa
hao!.Siku zilipita na mmaisha yakawa matamu kwa upande wao.Lakini leo nimepita
nyumbani kwao kuwajulia hali.Ila nilichokikuta na kukisikia nilishindwa
kukiamini lakini pia nimeshindwa kumshauri Jesca juu ya hili kutokana na hali
niliomkutanayo.Jesca niliemkuta leo sio yule niliemjua!hakuwa na furaha kiasi
cha kwamba nilijuta kwanini nilienda kuwajulia hali!.
Ukiachilia mbali mtoto ambae licha yakuwa amebebwa na
kubembelezwa na house girl ambae pia alipoteza furaha kwa hali iliyokuwa hapo
nyumbani.Kwa kweli hali nilioikuta ilinihuzunisha sana na nilijitahidi kuuliza
nini kilichojiri mpaka kukawa na hali hiyo,jibu la swali langu hilo
halikupatikana kwa urahisi kwani hata house girl ambae labda angeweza kuniambia
pia alikuwa hajui sababu iliyopelekea boss wake kulia!.
Baada ya jitahada za kutaka kujua nini kilichopelekea
shemeji yangu JESCA kulia hali ya kuwa yupo peke
Hatimaye alipunguza kilio chake na akaanza kunieleza kile
kilichopelekea yeye kulia kwa hasira na kwikwi na haya ndiyo aliyonieleza;
“Shemeji Hamisi huwezi kuamini na wala sikudhani kama mme
wangu ana tabia kama hizi!ama kweli kuwa uyaone na sasa nayaona!nilikuwa
nikijamini kuwa ninathamani na ninapendwa na mme wangu toka kipindi tupo chuo
lakini kumbe sikuwa na thamani kama ambavyo nilivyokuwa ninafikiria!Nimevuka
nguo!natamani ardhi ipasuke ili niingie nikajifiche!kweli Mungu hamfichi
mnafiki!sikufikiria wala sikudhani kama mme wangu anatabia hizi!naamini alikuwa
akifanya siri na sasa ameamua anionyeshe dhahiri!PETER!PETER!PETER wakunifanyia
mimi hivi!PETER wakufikia hatua ya kufanya hivi!leo naamini mapenzi hayana
mdhamana!kweli amini kuwa unapenda ila usiamini kama unapendwa!hivi upendo na
uaminifu wangu kwa mume wangu kweli nillistahili kuyakuta haya niliyoyakuta!”.
JESCA aliendelea kulalamika bila ya kuweka wazi kile
anachomaanisha,niliamua kumpigia simu rafiki yangu PETER ili anijuze kafanya
nini mpaka hali imekuwa hivi,lakini alishangaa na kutoamini kile ninachokiona
na kukisikia nyumbani kwake!baada ya kumthibitishia uhalisia wa kile
ninachokiona alianihakikishia kuwa anatoka ofisini muda si mrefu atakuwa
amefika nyumbani.
“Shemeji HAMISI naumia sana,sikustahili hiki!hivi PETER
wakuniwekea condom kwenye suruali yake!nimekuta condom hii ambayo haifunguliwa
na pakiti hii ya condom ambayo imetumika!”.
JESCA alinionyesha condom ambayo alidai ameikuta kwenye
mfuko wa suruali ya mumewe pindi alipokuwa anafua na pia alinionyesha pakiti ya
condom ambayo inaashiria kuwa condom yake ilitumika,
Hapa nilipo JESCA ameanza kulia tena kwa uchungu house girl
na anajitahidi kumbembeleza motto ambaye kila akimuangalia mama yake anayetokwa
na machozi nae anazidisha kilio na mama yake hawezi kumshika wala kumbembeleza
motto!sijuhi PETER atakuja kusema nini!wakati namsubiri nimeona nikushirikishe
ili unisaidie mawazo juu ya mkasa huu.Unaweza uvaa uhalisia wangu,JESCA au PETER
Toa maoni yako wakati tunamsubiri PETER atueleze kulikoni.
Comments
Post a Comment